Ofisa Habari wa Klabu ya Yanga, Ali Kamwe, amesema kuwa wao ni waungwana na wako tayari kucheza Dabi ya Kariakoo endapo watapewa maelezo ya kina kuhusu sababu za kuahirishwa kwa mchezo huo na Bodi ya Ligi Machi 8 mwaka huu. Amesema majibu hayo yatawasaidia wanachama wa Yanga kuelewa hali halisi na hivyo kupunguza hali hii ya sintofahamu.
Aidha, Kamwe ameongeza kuwa iwapo Klabu ya Simba itaeleza kwanini haikuleta timu uwanjani Machi 8, basi Yanga itakuwa tayari kushiriki mchezo huo utakaopigwa Juni 15, 2025.