Mchambuzi Hansrafael Aishangaa Bodi ya Ligi Kuleta Refa wa Misri Kuchezesha Dabi ya Kariakoo
Hapa najiuliza maswali mengi kwanini ligj yetu inaendeshwa kinyume na kanuni?🤔
Ni Kanuni Gani imetumika kuamua Derby ya Yanga vs Simba ichezeshwe na waamuzi kutoka nje ya nchi?
Kanuni namba 8 itazipa ruhusa ya kutoa malalamiko kwa maandishi kwenda TFF siku 3 kabla ya mchezo ikiwa hawajaridhishwa na Mwamuzi aliyepangwa,Je Simba na Yanga wameshirikishwa kwenye hili? KLABU ZINATAKIWA ZIJIBU HILI.
Ikitokea Timu moja ikagoma kuja uwanjani kwa madai kuwa Kanuni zimevunjwa,Watakuwa na haki je mechi namba 184,itaahirishwa tena?
4.Je,Timu itakayopoteza mchezo, ikikata rufaa kwa madai ya kuvunjwa kwa kanuni,Matokea yatafutwa?
Je Ni uamuzi kwa ajili ya “Ushirikiano”wa kimpira kati ya Tanzania na Misri? Je tumepima ubora wa waamuzi hawa ikiwa Derby ya Misri Klabu za Al Ahly na Zamalek zimegoma mechi yao isichezeshwe na waamuzi wa ndani? Tumeidharau Derby Yetu?
Je,Uamuzi huu uliokuja baada ya kukosekana kwa Refa Arajiga,aliye masomoni Unathibitisha kuwa LIGI YETU msimu huu imechezeshwa na Waamuzi wa hovyo zaidi wasiokidhi viwango vya mechi kubwa za Ligi?
Kamati ya Waamuzi haioni kama ina wajibika katika hili kwa kutengeneza marefa ambao hawana UWEZO wa kuchezesha mechi kubwa Derby?
Bodi ya Ligi na TFF wamefanya Uamuzi huu kwa HOFU gani? LIGI na MPIRA wa TANZANIA UMESHINDWA?
Kichwa changu kina maswali mengi….kwanini mpira wetu unakiuka kanuni na kuleta matatizo makubwa mbeleni?🤔
Hansrafael14