Simba Sc imeendelea kuvitafuna viporo vyake taratibu na hii leo wamechukua pointi zote tatu kufuatia ushindi mnono wa 5-1 dhidi ya TP Lindanda, Pamba Jiji Fc katika dimba la KMC Complex.
Jean Charles Ahoua amefunga hat-trick na kufikisha jumla ya magoli 15 kwenye Ligi Kuu bara mpaka sasa akiwa kinara wa ufungaji wakati Lionel Christian Ateba akifunga magoli mawili na kufikisha jumla ya magoli 12.
FT: Simba Sc 5-1 Pamba Jiji Fc
⚽ 15’ Ahoua (P)
⚽ 36’ Ahoua
⚽ 47’ Ahoua
⚽ 79’ Ateba
⚽ 84’ Ateba
⚽ 87’ Tegisi