Ahmed Ally Afunguka Watanzania Kuto Itendea Haki Taifa Stars Licha ya Kufanya Vizuri CHAN

Ahmed Ally Afunguka Watanzania Kuto Itendea Haki Taifa Stars Licha ya Kufanya Vizuri CHAN


 Ameandika ahmed ally

Tunakwenda kwenye hatua ya Robo Fainali ya CHAN dhidi Morocco August 22

Lazima tukiri kuwa hatua ya Makundi haikua bora kwetu kwenye upande wa majukwaa

Pamoja na timu yetu kuwa ndio timu iliyofanya vizuri kuliko zote lakini haijapata thamani sawa ya ubora huo na muitikio wa mashabiki

Sio muda wa kushikana uchawi bali ni muda wa kila mtu kutimiza majukumu yake

Kwenye kutimiza majukumu, Niwaombe ndugu zangu Waandishi wa habari nyie ni kiungo muhimu sana kwenye kufanikisha jambo lolote lile

Kwenye vipindi vyenu vya michezo ipeni nafasi Stars, tengenezeni morali kwa mashabiki na muwaite mashabiki waje Uwanjani

Watu mashuhuri wa kada zote tuibebe Agenda hii ya Taifa, tutumie nafasi zetu kuhamasisha mashabiki wetu twende Uwanjani

Mechi ya Robo Fainali tuvunje rekodi yetu ya kuingia Uwanjani na hilo linawezekana sana

Viongozi wa Matawi ya Simba, Azam, KMC na Yanga tumieni Matawi yenu kuhamasisha Wanachama wenu kuja kwa wingi Uwanjani

Vile mnfanya panapokua na mechi za vilabu vyetu tufanye hivyo hivyo kwa Taifa letu.

Ijumaa August 22 twendeni tukaujaze Benjamini Mkapa

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad