TRANSFER RUMOURS:
Yanga SC wapo hatua ya mwisho ya makubaliano ya kumsajili nahodha wa Simba SC Mohamed hussein kama mchezaji huru baada ya mkataba wake kumalizika.
Kipaumbele cha Hussein ni kubaki Simba SC ingawa hawajafikia makubaliano mazuri , ikiwa Zimbwe Jr atashindwa Kufikia makubaliano na Simba SC atajiunga na Yanga.
Makubaliano yake na Yanga SC yapo katika kiwango cha juu na wamekubaliana kusaini mkataba wa miaka miwili hadi kuwatumikia young Africans 2027.
Lolote linaweza kutokea kuanzia sasa kinachosubiriwa ni mchezaji huyo Kusaini Mkataba.