Tetesi za Soka Ulaya Jumamosi: Chelsea wanataka dau la £ 100m kwa Jackson

Tetesi za Soka Ulaya Jumamosi: Chelsea wanataka dau la £ 100m kwa Jackson


Chelsea waweka dau kubwa kwa Nicolas Jackson, Barcelona wamgeukia Marcus Rashford katika kumsaka winga mpya wa kushoto, Juventus wakubali kima fulani kwa ajili ya Jadon Sancho na mengine mengi.

Chelsea imeweka dau la pauni milioni 100 kwa mshambuliaji wa Senegal Nicolas Jackson, 24, huku AC Milan ikimtaka. (Mail)

Mchezaji wa Manchester United na Muingereza Marcus Rashford, 27, anafuatiliwa na Barcelona kama winga mpya wa kushoto baada ya klabu hiyo ya Uhispania kushindwa kumnunua mshambuliaji wa Liverpool na Colombia Luis Diaz, 28, na Mhispania mwenye umri wa miaka 22 Nico Williams wa Athletic Bilbao. (Sky Sports)

Juventus wamekubaliana mkataba wa euro 20m (£17.3m) na Manchester United kumnunua winga wa Uingereza Jadon Sancho, ambaye anafanya mazungumzo na klabu hiyo ya Old Trafford kabla ya uhamisho wowote. (La Stampa - in Italian)

Tottenham bado wanavutiwa na mchezaji wa kimataifa wa DR Congo Yoane Wissa, licha ya kuwa hawajawasiliana na Brentford baada ya kuambiwa kuhusu thamani ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 kuwa £50m mapema msimu huu wa joto. (Standard)

PSV Eindhoven wako tayari kumuuza winga wa Ubelgiji Johan Bakayoko, 22, huku Everton, Nottingham Forest na Bournemouth, pamoja na RB Leipzig na Bayer Leverkusen, wakionyesha nia ya kutaka kumsajili. (Fabrizio Romano)

Nottingham Forest inaweka dau la pauni milioni 25 pamoja na nyongeza kwa kiungo mshambuliaji wa England chini ya umri wa miaka 21 James McAtee lakini Manchester City wameweka thamani ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 kuwa karibu pauni milioni 40. (Mail)

Atalanta wanataka ofa ya angalau pauni milioni 50 ili kufikiria kumuuza beki wa kati wa Italia Giorgio Scalvini, 21, ambaye anasakwa na Newcastle United na Manchester United. (i paper)

Arsenal bado wanammezea mate winga wa Real Madrid na Brazil Rodrygo, 24, licha ya wao kufikia makubaliano ya kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Muingereza Noni Madueke, 23. (GiveMeSport).

Aston Villa wanakaribia kukamilisha dili la mlinda lango wa Uholanzi Marco Bizot mwenye umri wa miaka 34 kutoka Brest ya Ufaransa. (Athletic - subscription required)

Klabu ya Uturuki Fenerbahce inakaribia kupata dili la kumsaini kiungo mshambuliaji wa Uhispania Marco Asensio, 29, kutoka Paris St-Germain. (Football Italia)

Winga wa Colombia Daniel Munoz, 29, anatumai kuondoka Crystal Palace msimu huu wa joto licha ya kusaini kandarasi mpya mwezi Aprili pekee. (Mirror)

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad