Stephen Aziz Ki Anataka Bilioni 1.2 ili Abaki Kuichezea Yanga, KUMEKUCHA Huko

Stephen Aziz Ki Anataka Bilioni 1.2 ili Abaki Kuichezea Yanga, KUMEKUCHA Huko



Mchezaji wa Yanga, Stephen Aziz Ki, ana ofa mbili kutoka Al Ahly na Orlando Pirates. Hata hivyo, Aziz Ki ndiye aliyeamua kupunguza mahitaji yake ili kusaini na Yanga, akidai dola 500,000, ambazo ni sawa na TZS bilioni 1.295.

Hadi sasa, Klabu ya Yanga haijafikia kiasi hicho cha fedha, ingawa wapo tayari kumpa Aziz Ki dola 350,000 sawa na TZS milioni 907. Aziz Ki ameendelea kushikilia msimamo wake wa kudai dola 500,000 ili kusaini.

Kwa mujibu wa mwandishi wa habari za michezo nchini, @jr_farhanjr ameeleza, bado hakuna mkataba uliosainiwa kati ya Aziz na Yanga, huku jitihada za kukidhi mahitaji yake zikiendelea.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.