DAR ES SALAAM; KITENDAWILI cha nani atakuwa Kocha Mkuu mpya wa timu ya Yanga ya Dar es Salaam, kimetegulies usiku huu baada ya klabu hiyo kutambulisha Pedro Gonçalves raia wa Ureno kuwa ndiye atakinoa kikosi chao.
Wasifu wake unaonesha kuwa amepata kuzinoa klabu mbalimbali, lakini pia ameinoa timu ya Taifa ya Angola, anachukua nafasi ya Romain Folz aliyetimuliwa wiki iliyopita.
.png)
