Timu ya SIMBA Waendelea Kuhangaika Kumpata Mrithi wa Mohamed Hussein Zimbwe

Timu ya SIMBA Waendelea Kuhangaika Kumpata Mrithi wa Mohamed Hussein Zimbwe


Klabu ya Simbasc bado inaendelea kusaka mlinzi wa kushoto mwenye daraja la Mohamed Hussen ambaye atakuja kuziba nafasi hiyo

‎Mpaka sasa Simbasc tayari imepokea walinzi wawili wa kushoto ambao wanaendelea kuwafanyia majaribio kama wanaweza kukidhi mahitaji ambayo wanayahitaji

‎Tayari kwenye kambi yao nchini Misri yupo mlinzi wa kushoto kutoka Cameroon Jonathan Ngwem ambaye ni mchezaji huru kutoka kwenye kikosi cha Feature Fc ya nchini Misri

‎Pia Simbasc wamempokea mlinzi wa kushoto Hernest Briyock Malonga kwa maangalizi zaidi kama atawafaa

‎Itoshe kusema namba 3 kwenye kikosi cha Simbasc ni kizungumkuti mpaka sasa viongozi wanaumiza kichwa kumpata mbadala sahihi

‎Hii ni kutokana na pressure kubwa ambayo iko njee, kwani wakichukua bora mchezaji watu watahoji kwanini walikubali kumuachia Mohamed Husseni kama awana uwakika wa kumpata mbadala sahihi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad