Shaffih Dauda: Hakuna Beki wa Kulia Tanzania Mkali Kama Shomari Kapombe

Shaffih Dauda: Hakuna Beki wa Kulia Tanzania Mkali Kama Shomari Kapombe


Nimepata kuwashuhudia walinzi wengi wa kulia wakicheza soka kwenye ardhi hii ya Tanzania hapa nazungumzia wazawa na hata waliokuja wakitokea nje ya Tanzania


Lakini hayupo mlinzi wa kulia mwenye mwendelezo wa kiwango cha juu mechi baada ya mechi kumzidi Shomy , bado pia hayupo beki wa kulia hatari kwenye box la wapinzani kumzidi Kapombe


Kufunga sio jambo geni kabisa kwake , amefunga sana ligi ya ndani , amefunga pia kimataifa akiwa na klabu na bado anafunga Timu ya Taifa


Ukiwa na Shomari unapata uhakika eneo la ulinzi , unakuwa na matumaini ya kushuhudia assist muda wowote kutoka kwake na inapobidi basi anaimaliza mechi mwenyewe kama ilivyotokea hii leo

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad