TIMU ya Azam ni Kweli Wako Serious na Kocha Ibenge?

TIMU ya Azam ni Kweli Wako Serious na Kocha Ibenge?

SOKA letu limepiga hatua. Kuna mambo mengi yanayobadilika kwa kasi ambayo yanaashiria moja kwa moja tumeanza kuingia kwenye anga nyingine.

Ni mambo hayo ambayo yanatutofautisha kabisa na majirani zetu. Sasa hivi kwa Tanzania kuingiza timu nne kwenye mashindano ya kimataifa imekuwa ni kitu cha kawaida. Hata ukimuuliza shabiki wa mtaani kabisa ambaye hajui mpira anaona ni kitu cha kawaida, lakini siyo jambo jepesi, kuna kitu kimefanyika mahali kwa muda mrefu.

Achana na sifa ya ligi yetu kuwa kwenye nafasi za juu, hata klabu zetu na zenyewe sasa zimeanza kushindana na wakubwa kwenye renki za ubora wa Afrika. Hayo ni mafanikio ya kujivunia.

Makocha wakubwa, wachezaji wakubwa wanaiangalia ligi yetu. Leo hii gharama za timu kuwa bingwa zimeongezeka kuanzia aina ya kikosi ulichonacho mpaka benchi la ufundi.

Ndiyo maana utaona kwa sasa hata wachezaji wanaokuja kutoka nje ni wale ambao bado wanaf-ikiria miaka mingi mbele juu ya vipaji vyao. Tanzania imegeuka daraja la wao kwenda mbele kusaka utajiri na siyo sehemu ya kustaafia. Walimu wakubwa wenye sifa wanaitamani Tanzania sasa. Tunapozu-ngumza hapa, Mkong-omani Florent Ibenge tayari yupo Tanzania.

Anafu-ndisha mpira Mbagala. Fungu la Azam timu yenye utajiri mkubwa zaidi wa rasilimali nchini imempa kazi ya kuhakikisha anawavusha kutimiza malengo yao hasa katika Kombe la Shirikisho Afrika msimu ujao.

Ni kocha ambae wasifu wake unatosha kushawishi watu wengine kutaka kuijua ligi yetu. Hakuna kitu ambacho hajafanya kimataifa. Tena akiwa na timu kubwa.

Ligi yetu imetawaliwa na timu mbili za Kariakoo kwa maana ya Simba na Yanga, lakini ujio wa Azam unaon-ekana kuwapa matu-maini wengi kama timu itakayo-utoa mpira wetu kwenye makucha ya miamba hiyo miwili.

Siyo kazi rahisi ya kutamka tu mdomoni lakini lazima ianze sehemu kutokana na mizizi iliyowekwa na miamba hiyo ya Kariakoo. Azam hawako mbali sana kwani kwa miaka kadhaa wameweza kukaa katikati yao na kilichobaki ni kukaa juu yao kwa kuwatumia watu wenye maono mak-ubwa kama Ibenge.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad