Meneja wa habari na mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amesema kuwa usajili wa klabu hiyo msimu huu umejikita zaidi kwenye umakini wa ICU.
''Mitandaoni na kwenye vyombo vya habari kuna taarifa za usajili kuhusu Simba wengine wanaihusisha Simba kwenye kila mchezaji ili kuwapa thamani Wachezaji wanaotaka kuwasajili”
“Taarifa tu ni kwamba usajili wetu safari hii unafanyika kwa umakini wa ICU, na Wachezaji waliopendekezwa na Mwalimu wameshasajiliwa na wengine wapo kwenye hatua za mwisho za kukamilisha usajili. Kwa sasa tunamalizia kutoa barua kwa wale tunaochana nao kisha tuanze kuvurumisha Thank You na baada ya hapo tuanze kudondosha chuma kimoja baada ya kingine'' Ahmed Ally