Mzize Sasa Njia Nyeupe Kwenda Zamaleki, Wapagawa na Kiwango Chake

 

Mzize Sasa Njia Nyeupe Kwenda Zamaleki, Wapagawa na Kiwango Chake

Taarifa zinabainisha kuwa, Yanga imekubaliana na Zamalek ya Misri inayotaka kumsajili Mzize kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kufikia muafaka wa maslahi kwa pande hizo sambamba na uongozi unaomsimamia mchezaji anayehusishwa na klabu za Ufaransa na Morocco wiki kadhaa zilizopita.


Bosi mmoja wa juu kutoka Yanga, amefichua kuwa Zamalek imekubali kutoa Dola 750,000 (Sh2 bilioni) kumnunua mshambuliaji huyo aliyebakiza mkataba wa miaka miwili kikosini hapo.


Inaelezwa kwamba, Zamalek italipa fedha hizo kwa mafungu mawili ambapo kutakuwa na malipo yatakayofanyika kabla ya mchezaji huyo kuondoka kisha awamu ya pili yatafanyika Januari 2026 ambapo pande hizo mbili zimekubaliana.


Malipo ya kwanza ya mauzo hayo yatakayofanyika ni dola 375,000 (Sh991 milioni), kisha kiasi kama hicho kitalipwa baadaye kukamilisha makubaliano yaliyopo kufanya jumla kuwa ni dola 750,000.


Awali ilielezwa Mzize alikuwa na ofa nyingi za hukohuko Afrika Kaskazini kwa mataifa ya Morocco, Libya na hata Ulaya lakini Zamalek ndio ilikuwa kinara kwa kufikia makubaliano mazuri na Yanga.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad