Kwa upande wa pili kuna Simba SC, klabu yenye misuli ya historia lakini ina moyo wa kisasa. Wanatoka kwenye ushindi wa kihistoria dhidi ya Al Masry, wakipindua meza kutoka 2-0 hadi kushinda kwa penalti 4-1, baada ya kupata matokeo ya 2-0 nyumbani jijini Dar es Salaam.
Wanakuja kwenye mchezo huu wa nusu fainali wakiwa na nyota kama Steven Mukwala, mshambuliaji hatari, na Elie Mpanzu, mchezaji mwenye mvuto na ubunifu wa aina yake.
Simba si wageni wa hatua hii, lakini wana kiu ya kutwaa taji la Afrika. Ni timu inayobeba shinikizo la historia, lakini pia silaha ya uzoefu wa miaka na miaka kwenye mashindano ya kimataifa.
"Simba wamecheza na timu kubwa zaidi ya Stellenbosch, Stellenbosch hawapo 'Level' (kiwango) ya Al Ahly, Zamalek, Wydad ata Kaizer Chiefs kwahiyo naamini Simba hawana hofu na Stellen bali wanawaheshimu tu" anasema George Ambangile, Mchambuzi wa soka Tanzania.