Bacca Aibeba Bendera ya Wazawa Mbele ya Wasauzi, Usajili Unaoendelea Kulipa Siku Hadi Siku

Published from Blogger Prime Android App


IBRAHIM ABDALLAH BACCA, anazo stori kuhusu bendera ya Wazawa kisha anazo simulizi za kuipeperusha bendera hii! Leo tena aliwaambia sitofanya hivyo nje ya uwanja bali ndani, bendera ya Wazawa inapepea kwa jasho na damu mbele ya Madiba! Thats it, thats the post!

Walisema ni mchezo ambao hautabiriki! Kocha Nabi aliingia na mavazi ya chakula cha usiku, lakini Bacca alibeba kadi ya kuchanja! Wananchi wote kuleni na kusaza, kunyweni na kujigalagaza kama kwa Shishi wa Igunga kisha bills juu yake, eat and drink the bills on him alimaanisha hilo.

Sajili haikueleweka hii kama Katuni za Masoud Kipanya, Mchezaji hakueleweka huyu kama Masha Love na Jimmy Mafufu, wakasema ni viatu vikubwa sana kwake kuvaa lakini Afande aliwaambia miguu inatosha, kiatu ni kizuri nipeni jezi ya Yanga nivae nikue naye! La kuchumpa lako mpe Bacca, its show time.

Mpira mkubwa sana kutoka kwa Afande, Marumo walikuja na Amapiano ila aliishi kiapo chake kwa Jamhuri kuwa NEMC hawataki kelele, Wavuvi na Kitambaa zimefungwa, akaamrisha spika za Amapiano zishushwe na Wasauzi waondoke mikono nyuma, haikuwa ombi ni amri! Try Again later kama Simba na Azam, ooh sorry kama Mazembe na Club Africain.

KARIBU ZANZIBAR ilisomeka! Nyumbani kwa Nadir Haroub Ally Upapa aliyekuwa Papa Jangwani, nyumbani kwa Abdi Kassim Babi aliyekuwa Shabaab lakini ndio nyumbani kwa Kitasa na Mudathir, Legendary status in the making! Mdogo mdogo kama Vicoba na Upatu, taratibu zinapanda kama genye na bia kwenye baridi kali😀

Bacca mmoja mpirani, Bacca mmoja nyumbani rimotini! Zima redio mbao, zima na mitandao, watakufa kwa mshangao! They see us, they hear us IMAGINE BEING MWANANCHI🔰

VISIT MOROGORO🇹🇿

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.