Klabu ya Yanga leo inaingia kifua mbele kuikabili Simba ambayo itaingia kama timu ya pili (underdog) kitakwimu kutokana na matokeo ya nyuma.
Yanga kwenye michezo mitano (5) ya mwisho ya mashindano rasmi mbele ya Simba imeshinda yote huku Simba ikiambulia patupu.
Katika michezo hiyo mitano (5) Yanga imefunga magoli 11, huku Simba ikifunga magoli mawili (2) pekee.
Makocha wa timu zote mbili hawajawahi kukutana, huu ndio utakuwa mchezo wao wa kwanza kukutana