HATIMAYE Mo Dewji Ajitokeza na Kusema Haya Kuhusu Mwendendo wa Timu ya Simba

HATIMAYE Mo Dewji Ajitokeza na Kusema Haya Kuhusu Mwendendo wa Timu ya Simba


Wapenzi wa Simba,

Najua mioyo yenu imebeba maswali mengi. Kama Rais wenu, msione nimekaa kimya wakati tumepitia kipindi hiki kigumu. Kupambania Simba ni wajibu wangu.

Huu siyo wakati wa lawama ni wakati wa kusimama imara, kuwa kitu kimoja, na kuchukua hatua sahihi za kuleta mabadiliko chanya.

Katika siku chache zijazo, nitazungumza na nyie moja kwa moja. Kuna kazi kubwa inaendelea, na kuna matumaini ya kweli.

Simba haijapotea. Tumekuwa kwenye kipindi cha mpito, tumejenga kikosi kipya, tumeimarisha benchi la ufundi, na tumeweka msingi wa mwelekeo mpya. Msimu huu tumefika mbali zaidi ya matarajio, na msimu ujao tunarudi kwa nguvu mpya.

Naomba tuendelee kuwa wavumilivu. Tunahitaji kufanya marekebisho makubwa. Tuendelee kusimama pamoja kama familia moja.

Mbele yetu kuna mwanga. Na kwa pamoja, tutarudi tukiwa imara zaidi, wenye njaa zaidi, na wa kishujaa zaidi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad