Azam yaizamisha KMKM kwa bao 5-2, sasa kukutana na Simba

Azam yaizamisha KMKM kwa bao 5-2, sasa kukutana na Simba

Timu ya Azam Fc imefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya kombe la Muungano mara baada ya kupata ushindi wabao 5-2 dhidi ya timu ya KMKM SC ya visiwani Zanzibar.

Mabao ya Azam yamefungwa na Abdul Sopu dakkka ya 7 na 42, Chilambo dakika ya 9, Idd Nado dakika ya 49 na Kishindo dakika ya 74.

Mabao mawili ya KMKM yamefungwa Abdurahman Alli dakika ya 38 na dakika ya 65 bao la mkwaju wa penati.

Azam FC sasa watacheza dhidi ya Simba SC katika hatua ya fainali ya Muungano Cup Jumamosi ya April 27 2024 katika uwanja wa New Amaan Complex Zanzibar.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.