KIUNGO wa Azam FC, Feisal Salum amekata mzizi fitna kuhusu maneno yanayoendelea kusemwa kwamba huenda akatimikia Simba, akifunguka kuwa kama ataondoka anapocheza sasa basi hawezi kujiunga na timu yoyote Bongo ikiwamo ya Wekundu wa Msimbazi.
Fei ambaye aliwahi kuichezea Yanga kwa mafanikio, ameendeleza moto wake hadi alipojiunga na Azam ambako alisaini mkataba wa miaka mitatu ambao unaisha msimu ujao.