Kwa niaba ya wachezaji Nahodha wa timu ya Taifa Mohammed Hussein “Tshabalala” amemshukuru Rais Dkt. Samia kwa kuwezesha kupatikana kwa usafiri wa ndege kwa ajili ya mchezo dhidi ya Congo.
“Kwetu sisi hii ni motisha kuelekea michezo yetu miwili dhidi ya Congo, kwasababu itatusaidia kurejea haraka nyumbani kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa marudiano”. Mohamed Hussein, Mlinzi wa kushoto wa Timu ya Taifa ya Tanzania.