Ni Ahly Vs Mazembe, Mamelodi Vs Esperance Nusu Fainali Ligi ya Mabingwa Afrika

Ni Ahly Vs Mazembe, Mamelodi Vs Esperance Nusu Fainali Ligi ya Mabingwa Afrika


Timu za TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Esperance ya Tunisia zimefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuzitoa ASEC Mimosas ya Ivory Coast na Petró Atletico Luanda ya Angola. Mazembe jana ilipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji, Petró Atletico Uwanja wa Novemba 11 Jijini Luanda, hivyo kusonga mbele kufuatia sare ya bila kwenye mchezo wa kwanza Lubumbashi wiki iliyopita.


Katika mchezo wa jana, Petró Atletico walitangulia kwa bao la mshambuliaji wa Honduras, Jonathan Toro dakika ya 29, kabla ya Mazembe kutoka nyuma kwa mabao ya washambuliaji Philippe Kinzumbi dakika ya 82 na Joël Beya dakika ya 90.


Mazembe sasa itakutana na Al Ahly ambayo iliitoa Simba na Tanzania kwa jumla ya mabao 3-0, ikishinda 1-0 ugenini na 2-0 nyumbani.


Kwa upande wao Espérance jana walilazimisha sare ya 0-0 na wenyeji, ASEC Mimosas Uwanja wa Félix Houphouët-Boigny Jijini Abidjan, kabla ya kushinda kwa penalti 4-2 kufuatia sare ya 0-0 pia kwenye mchezo wa kwanza Tunisia.


Esperánce sasa itakutana na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini ambayo iliitoa Yanga ya Tanzania kwa penalti 3-2 kufuatia sare ya 0-0 ugenini na nyumbani.


Mechi za kwanza za Nusu Fainali zitachezwa Aprili 19 na marudiano Aprili 26, Mazembe na Esperance wakianzia nyumbani.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.