Uchambuzi Mechi ya Simba na KMC, Simba Ufanisi Ulikuwa Mdogo, KMC Game Bora Sana

Uchambuzi Mechi ya Simba na KMC, Simba Ufanisi Ulikuwa Mdogo, KMC Game Bora Sana

Uchambuzi Mechi ya Simba na KMC, Simba Ufanisi Ulikuwa Mdogo, KMC Game Bora Sana


Simba na 4-2-3-1 kama kawaida yao , walianza mchezo wakiwa chini sana : wanafanya makosa mengi hasa wakishambulia (wanapoteza pasi kirahisi , movements zao hazikuwa sahihi , hawakuwa na maamuzi ya pasi za mwisho + ufanisi ulikuwa mdogo .

Kmc na mikakati ya kuzuia kwanza then washambulie kwa kushtukiza : Nafikiri ndio ulikuwa mtego wao sahihi hasa mbele ya Simba , Walifanikiwa hasa kipindi cha kwanza ( wakipora mipira wanaunda mshambulizi kwa haraka “Counter Attacks” walichokosa ni ufanisi na maamuzi . DECISION MAKING . Kwa kipindi cha kwanza Kmc wangeweza kuondoka hata na goli zaidi ya moja .

Kipindi cha pili , Simba waliongeza ufanisi mbele ya goli , walifanya vitu vya kimsingi sana : Pasi sahihi , Movements , Ufanisi . 2-4-3-1 wakati Simba wanashambulia (Saido Kibu na Mzamiru nyuma ya Baleke then Zimbwe na Kapombe mstari mmoja na wale viungo wawili Ngoma na Kanoutè ) waliwaruhusu FBs kusogea juu zaidi + Kibu anaingia kwenye “Half Spaces” na Mzamiru mda mwingi alicheza ndani kwenye kiungo . Simba walitengeneza idadi kubwa ya wachezaji wakati wanashambulia .

Nafikiri kama Kmc wangekuwa na maamuzi sahihi kwenye eneo la mwisho basi walikuwa na nafasi ya kuimaliza game mapema kipindi cha pili . Kuna nyakati ni wao tu kuweka mpira kwenye nyavu ( Elias , Awesu , Makang’a Wazir Jr walikosa maamuzi wakifika kwenye eneo la mwisho .

NOTE:

Wazir Jr kwenye nyakati sahihi ✅

Wale Kmc wakiwa na mali 👏🔥 Watulivu sana ✅ Awesu , Ibrahim Elias 🔥

Maseke amecheza game bora👏 …. Kapombe ✅ Kibu D anaubonda sana aisee 🔥

FT: Kmc 2-2 Simba

By Kevinrabson 


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.