Kuelekea Mechi ya Simba na Azam, Azam Waweweseka.. Kocha Ongalla Afunguka Kuwafanyia Tizi Kali la Kufa Mtu

Kocha Ongalla Azam

Kuelekea Mechi ya Simba na Azam, Azam Waweweseka.. Kocha Ongalla Afunguka Kuwafanyia Tizi Kali la Kufa Mtu

Mtwara | Kocha Msaidizi wa Azam FC Kali Ongala amsema, timu yao ilipata fursa ya kucheza mechi mbili za kirafiki ili kuwaweka tayari wachezaji kuelekea mchezo wa Nusu Fainali ya Azam Sports Federation Cup dhidi ya Simba.


“Tumecheza mechi mbili za kirafiki ambazo hazihusishi mashabiki [behind closed doors] kwa ajili ya kuwapa wachezaji utayari wa mechi.”


“Tupo kwenye kipindi ambacho tunaelekea mwishoni mwa msimu, wachezaji wameshapitia mambo mengi kuanzia pre-season hadi hapa walipo, ndio maana hata wenzetu kikosi chao kilichocheza juzi kilikuwa na mabadiliko makubwa.”


Mara ya mwisho Azam kucheza mechi ya ushindani ilikuwa ni Aprili 22, 2023 [Ruvu Shooting 1-3 Azam FC], Ongala amesema anawaamini wachezaji wake na timu yake kuelekea mchezo wa kesho.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.